Home » » ASKOFU WA ANGLICAN DAYOSISI YA NJOMBE AFARIKI DUNIA

ASKOFU WA ANGLICAN DAYOSISI YA NJOMBE AFARIKI DUNIA

Written By kitulofm on Tuesday, 26 November 2013 | Tuesday, November 26, 2013

Askofu John Simalenga (Pichani) wa Dayosisi ya Njombe Kanisa la Anglikan Amefariki Dunia Asubuhi ya Saa Kumi na Moja Novemba 24 Mwaka Huu na Mazishi Yanatarajiwa Kufanyika Novemba 28 Katika Kanisa Hilo.
 
Taarifa Toka Kwa Msaidizi wa Askofu Huyo Mchungaji Canon Mlelwa Amesema Kuwa Marehemu Simalenga Amefariki Dunia Baada ya Kuugua Kwa Kipindi Kifupi Kwa Ugonjwa wa Malari na Kisukari Alichogundulika Kuwa Nacho na Hivyo Hadi Kifo Chake Kinamkuta Alikutwa na Malari Mbili.

Aidha Mlelwa Amesema Kuwa Marehemu Askofu Simalenga Amekufa Akiwa na Miaka 60 Ambapo Alizaliwa Mwaka 1953 Katika Kijiji cha Milo Wilayani Ludewa na Uaskofu Alipata Julai 7 Mwaka 2007 Kisha Kuwa Askofu wa 7 Wa kanisa Hilo.
 
Marehemu Askofu Simalenga Ameacha Watoto Wanne na Mjane Mmoja. 
Taarifa zaidi Juu ya Msiba Huoendelea kutembelea mtandao huu
 
Na Gabriel Kilamlya
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm