Na Veronica Mtauka
Mafunzo ya ulinzi na usalama
wa mtoto dhidi ya ukatili na unyanyasaji yameanza kutolewa katika ukumbi wa
Sumasesu kata ya Tandala wilayani Makete Mkoani Njombe kuanzia hapo jana
Mafunzo hayo yaliyofunguliwa
rasmi ha;po jana na Afisa Ustawi wa jamii wilaya ya Makete Bw.Leonce Panga
ambapo yamehudhuriwa na wadau mbalimbali pamoja na viongozi wa dini,dawati la
jinsia kutoka kituo cha polisi Makete,maafisa elimu, magereza,mwanasheria wa
halmashauri ya wilaya, ,wauguzi, pamoja na Mh.hakimu mfawidhi wa wilaya ya
Makete
Katika mafunzo hayo
wawezeshaji walikuwa ni Bi.Asha Mbaruku pamoja na Ramadhani Yahaya kutoka
kutoka ustawi wa jamii makao makuu jijini Daresalaam ,wawezeshaji hao wamesema
kuwa lengo la mafunzo hayo kwa wadau waliohudhuria ni kuwajengea uwezo
washiriki namna ya kuwahudumia watoto
Washiriki hao wametakiwa kuwa
timu ya ulinzi kwa na usalama kwa mtoto ili waweze kumsaidia mtoto,pia Bi.Asha
amesema kuwa kuna huduma ya msaada kwa mtoto aliyefanyiwa ukatili limeanzishwa
wizarani ambapo inaitwa huduma mtandao (CHILD HELPLINE) inayohusu mtoto kupiga
simu moja kwa moja na kueleza shida yake na kutafutiwa suluhu
Washiriki hao pia
wamefundishwa mbinu mbalimbali za ufundishaji wa masuala ya ulinzi na usalama
wa mtoto kwa ngazi ya chini ya serikali
Kwa upande wao washiriki
wametoa visa mbalimbali vinavyoendelea katika jamii yetu kama
kata ya Mbalatse watoto wa kike kufanyiwa ukeketaji kwa siri
Mafunzo hayo pia yaliweza
kuweka wazi kuhusu nini serikali imefanya dhidi ya ulinzi wa usalama wa mtoto
katika masuala ya ukatili kama kutengeneza
sheria ya mtoto ya mwaka 2009 kuridhia mikataba mbalimbali ya kimataifa kikanda
inayohusu masuala ya ukatili dhidi ya watoto
Mafunzo hayo ya siku 5
yaliyoanza siku ya jana yameandaliwa na ustawi wa jamii makao makuu Daresalaam
na yanatarajiwa kumalizika wiki hii siku ya jumamosi
0 comments:
Post a Comment