Home » » MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAKETE ATANGAZA KUGOMA KUPOKEA MRADI WA MAJI TARAFA YA MATAMBA

MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAKETE ATANGAZA KUGOMA KUPOKEA MRADI WA MAJI TARAFA YA MATAMBA

Written By kitulofm on Sunday, 17 November 2013 | Sunday, November 17, 2013



 Mradi wa maji uliopo Matamba.

Kutokamilika kwa baadhi ya miradi ya maji na mingine kujengwa chini ya kiwango kumeonekana kuwa mwiba mchungu kwa wananchi na baadhi ya viongozi wapenda maendeleo wilayani Makete mkoani Njombe

Hayo yamebainika kwenye kikao cha kamati ya ushauri ya wilaya (DCC) kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Makete wilayani hapa

Akizungumza kwenye kikao hicho, mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Makete Mh. Daniel Okoka amesema kwa upande wa tarafa ya Matamba amesema yeye kama mtia saini mikataba ya ujenzi wa miradi hiyo hataipokea mpaka akatapofanya ukaguzi hatua kwa hatua

"Mimi nitakwenda Matamba na kuwafuata wananchi tunakwenda hatua kwa hatua na kuzungumza nao wakati wa ukaguzi na wakiridhika na ujenzi huo wa mradi, mimi nitaupokea wakikataa sitaupokea" alisema Okoka

Amesema kwa kiasi kikubwa anashangazwa na baadhi ya viongozi wa Matamba ambao hakuwataja kumwambia kuwa hana mamlaka ya kufanya mikutano kwenye maeneo hayo, na kufafanua kuwa yeye kama mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Makete ana uwezo wa kufanya mikutano sehemu yeyote ile ndani ya wilaya yake bila kizuizi, na hivyo viongozi hao wasimkwamishe

Akichangia hoja hiyo, katibu wa CCM wilaya ya Makete Miraji Mtaturu amesema ni aibu kwa viongozi pindi miradi ya maji inapoonekana kutokamilika ilihali taarifa zinazotolewa zinaonesha kuwa miradi hiyo imefanyika na imekamilika 

Akizungumzia mradi wa Matamba amesema hali ni mbaya kwani mradi huo hautoi maji licha ya taarifa kudai kuwa umekamilika, na kudai kuwa huu si muda wa kulumbana kumtafuta mchawi na badala yake kinachotakiwa ni maji yawafikie wananchi na si kitu kingine

Naye mwenyekiti wa kikao hicho ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Makete Josephine Matiro ameagiza kuwa tatizo hilo la ukosefu wa maji katika maeneo mbalimbali yenye changamoto ikiwemo Matamba lifanywe haraka iwezekanavyo ukizingatia kuwa serikali imetoa kipaumbele kwa miradi hiyo ya maji
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm