Home » » UKATILI NA UNYANYASAJI KWA WATOTO WILAYANI MAKETE KUPUNGUA

UKATILI NA UNYANYASAJI KWA WATOTO WILAYANI MAKETE KUPUNGUA

Written By kitulofm on Friday, 29 November 2013 | Friday, November 29, 2013



Na Veronica Mtauka
Wadau wametakiwa kujua mbinu mbalimbali za kuwasiliana na mtoto mwenye matatizo ili waweze kuwasaidia watoto

Hayo yamesemwa na muwezeshaji Bi.Asha Mbaruku kwenye mafunzo ya ulinzi na usalama wa mtoto kwenye ukumbi wa sumasesu Tandala wilayani hapa mapema hii jana

Katika mafunzo hayo Bi.Asha amesema kuwa washiriki pamoja na wadau wanatakiwa kufahamu na kutambua njia za kuwasiliana na watoto wenye matatizo mbalimbali hasa ya ubakaji na kulawitiwa

Amesema wakati wa kuwasiliana na mtoto wadau wanatakiwa kuangalia kauli zao ili mtoto aweze kuelezea unyanyasaji aliofanyiwa na mtu au watu,pia wadau hao wametakiwa kufahamu ratiba ya mtoto wakati wa mawasiliano ili kuondoa usumbufu kwa mtoto na kuzingatia usiri wakati wa kuwasiliana nao

Aidha amesisitiza washiriki wa mafunzo hayo pamoja na watu wa ustawi wa jamii kuangalia mambo ya kimila kwa mtoto,suala la kidini,ulemavu,pamoja na umri wa mtoto ambaye unafanya nae mawasiliano na wasipende kumsemea mtoto katika matatizo yake kwa mujibu wa sheria

Mafunzo hayo ya ulinzi na usalama wa mtoto yanaendelea huku washiriki wakifundishwa mada mbalimbali za kupinga unyanyasaji na ukatili dhidi ya watoto ambapo mafunzo hayo yameandaliwa na ustawi wa jamii makao makuu Dar es salaam
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm