Home » » WAJASILIAMALI WILAYANI MAKETE WAOMBA KUPUNGUZIWA USHURU

WAJASILIAMALI WILAYANI MAKETE WAOMBA KUPUNGUZIWA USHURU

Written By kitulofm on Tuesday, 12 November 2013 | Tuesday, November 12, 2013



MAKETE
 Na:-Fadhil Lunati 

Wajasiliamali wadogowadogo wilayani makete mkoani Njombe wanaofanya biashara katika soko kuu la Iwawa wameomba kupunguziwa ushuru kwani kipato wanachopata hakiendani na ushuru wanaotozwa nakuomba wapunguziwe iwe sh.4000-6000 ikiwa ni pamoja na fedha ya mlinzi badala ya sh.8000 wanayolipa kwa hivi sasa.

wakizungumza na kitulo fm mapema hii leo wajasiliamali hao wamesema ushuru wanaotozwa hauendani na kipato wanachopata kwani hali ya usafirishaji wa bidhaa hizo ni ghali sana kutokana na miundombinu ya barabara iliyopo kuwa mibovu kutokana na vifusi vilivyo mwagwa kutosambazwa kwa wakati.

Aidha wajasiliamali wamezungmzia kero ya muda mrefu ya kuvuja kwa soko hilo kwabaadhi ya sehemu kwani walisha lalamika kwa uongozi husika lakini bado halijatekelezwa mpaka sasa.


Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm