Home » » WANAFUNZI MAKETE WAMETAKIWA KUJUA NJIA ZA KUPAMBANA NA RUSHWA

WANAFUNZI MAKETE WAMETAKIWA KUJUA NJIA ZA KUPAMBANA NA RUSHWA

Written By kitulofm on Thursday, 5 December 2013 | Thursday, December 05, 2013

Na Furahisha Nundu

Elimu ya kuzuia na kupambana na rushwa inazidi kutolewa katika makundi mbalimbali wilayani Makete likiwemo kundi la wanafunzi wa ngazi zote

Akitoa elimu hiyo kwa wanafunzi wa chuo cha St.Augustine Mkuu wa TAKUKURU wilaya ya Makete Bw.Daudi Joshua ameelezea njia za kuzuia na kupambana na rushwa ikiwa rushwa ni Chanzo cha kushuka kwa maadili na kusababisha kuporomoka kwa uchumi katika Taifa zima

Amesema kuwa wanafunzi katika ngazi tofauti wamekuwa wakikumbana na rushwa aina mbalimbali ikiwemo ya ngono ili kupata jambo Fulani kitu ambacho ni hatari katika taasisi ya TAKUKURU hivyo wawe makini katika kusababisha na kuzuia rushwa

Zaidi ya wanafunzi 16 wamepatiwa mafunzo hayo ikiwa kwa upande wa wanafunzi wenyewe wameshukuru kwa Taasisi hiyo kwa kutoa elimu hiyo ambapo taasisi hiyo ilianza mwaka 2007 kuunda vilabu vya kuzuia na kupambana na Rushwa katika shule za Sekondari wilayani hapa hata hivyo taasisi hiyo inampango wa kuunda vilabu katika shule za msingi zilizopo wilayani Makete

Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm