Home » » MBUNGE WA JIMBO LA MAKETE AMEGAWA VITABU ZIADI YA 200 SHULE YA SEKONDARI BULONGWA

MBUNGE WA JIMBO LA MAKETE AMEGAWA VITABU ZIADI YA 200 SHULE YA SEKONDARI BULONGWA

Written By kitulofm on Thursday, 9 January 2014 | Thursday, January 09, 2014

                       
 
Mbunge wa wilaya ya Makete Mh.Binilith Mahenge ameendelea na zoezi la ugawaji wa vitabu ktk shule za Sekondari zilizopo Wilani Makete ambapo leo hii amegawa zaidi a vitabu mia mbili ktk shule ya sekondali Bulongwa

Akikabidhi vitabu hivyo kwa mkuu wa shule hiyo Aksoni Ntulo mbele ya wananchi Mahenge amewasihi wazazi na walezi wa watoto kuwapeleka wanafunzi waliochaguliwa kuiunga na masomo ya sekondari kaika shule walizochaguliwa.


 Kwa upande wake Mkuu wa shule ya sekondari Bulongwa Mwl.Aksoni Ntulo amemshukuru Mh.Mbunge kwa msaada wa vitabu hivyo kwani hivi sasa anauhakika shule yake itaongeza ufaulu kwa wanafunzi kulingana na vifaa vya shule kuongezeka hivyo kila mwanafunzi atakuwa na uhakika wa ksoma kwa raha bila kung'ang'aniana vitabu pindi wawapo Darasani

Hata hivyo Penye nia pana njia japo kila penye mafanikio hazikosi changamoto kwani shule hiyo inakabiliwa na   changamoto kubwa ya upungufu wa vifaa vya maabara.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm