Home » » MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI MAKETE YAPUNGUA

MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI MAKETE YAPUNGUA

Written By kitulofm on Tuesday, 25 March 2014 | Tuesday, March 25, 2014

Picha na Edwin Moshi 

Sifa ya mbaya ya wilaya ya Makete Mkoani Njombe kuwa na idadi kubwa ya maambukizi ya virusi vya Ukimwi kwa miaka mingi sasa imeanza kuwa sifa nzuri baada ya Mkuu wa Mkoa wa Njombe Kapten Asseri Msangi kuuleza umma wa wanamakete kuwa idadi ya maambukizi ya virusi vya Ukimwi wilayani Makete inaendelea kupungua mwaka hadi mwaka

Sifa nzuri ya kuashiria kwamba wanamakete hivi sasa wameelimika kuhusu maambukizi ya virusi vya Ukimwi inazidi kupungua imeonekana kuwafurahisha wanamakete kwani wengi wao walikuwa na wasiwasi kila wanapokuwa wanafikiri kuhusu gonjwa hili Hatari la Ukimwi kwani limesababisha watoto wengi kuishi mazingira ya watoto yatima na Magumu

Kauli hiyo ilizungumzwa na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Asseri Msangi katika maadhimisho ya siku ya Maji Duniani ambapo mkoani Njombe maadhimisho hayo yalifanyika katika Wilaya ya Makete katika viwanja vya Mabehewani Makete Mjini mnamo tarehe 22 March 2014

Hata hivyo Msangi amesema kuwa mpaka sasa bado wilaya ya Makete imeendelea kukumbwa na changamoto kubwa ya kuwa na watoto yatima  wengi ambao wazazi wao kwa kiasi kikubwa walikufa kwa maambukizi ya virusi vya Ukimwi Ukimwi


Hivyo Kitulofm blog na Kitulo fm Redio inatoa rai kwa wanamakete kuishi kwa tahadhari juu ya maambukizi ya Virusi vya Ukimwi wasibweteke na sifa nzuri ambayo wameanza kuipata sasa badala yake wakawa makini ili kutokomeza kabisa gonjwa hili hatari la Ukimwi  

Na Furahisha Nundu
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm