Home » » KIWANGO CHA ELIMU SEKONDARI YA LUPALILO WILAYANI MAKETE CHAONGEZEKA

KIWANGO CHA ELIMU SEKONDARI YA LUPALILO WILAYANI MAKETE CHAONGEZEKA

Written By kitulofm on Monday, 25 November 2013 | Monday, November 25, 2013

Wanafunzi wa shule ya sekondari Lupalilo iliyopo wilayani Makete wameelezea kupanda kwa kiwango cha Taaluma kwa wanafunzi shuleni hapo

Wakizungumza na kitulo fm katika kipindi cha skuli club kinachorushwa kila siku ya juma mosi saa 1:15usiku-2:00 usiku ambapo wamesema kuwa kiwango cha ufaulu kwa
wanafunzi umeongezeka kutoka asilimia 65-kufikia 90 kulingana na jitihada za walimu pamoja na kujisomea wanafunzi wenyewe pindi wanapokuwa shuleni na majumbani
 

Shule hiyo inayoongozwa na Mwalimu mkuu Liombo yenye zaidi ya wanafunzi 600 na walimu 25 na masomo yanayofundishwa shuleni hapo ni sayansi pamoja na sanaa ikiwa shule hiyo ina mazingira yenye mvuto kwa kujisomea wanafunzi

Wakizungumzia suala la baadhi ya wanafunzi wa kike kupata mimba wawapo shuleni wamesema kuwa baadhi ya shule mazingira wa wanafunzi wa kike kuishi nje ya bweni ni moja ya sababu zinazofanya mwanafunzi kupata mamba

Hata hivyo wamewataka wanafunzi wengine nchini kujikinga na suala hilo na kupunguza utoro shuleni ili kuongeza kiwango cha elimu wilayani hapa na nchi nzima
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm