Home » » MAADHIMISHO YA SIKU YA CHOO DUNIANI MKOANI MWANZA.

MAADHIMISHO YA SIKU YA CHOO DUNIANI MKOANI MWANZA.

Written By kitulofm on Tuesday, 19 November 2013 | Tuesday, November 19, 2013


Mila potofu zimetajwa kuchangia kwa asilimia kubwa maambukizi ya maradhi yatokanayo na kukiuka kanuni za afya na usafi, likibainika katika utafiti uliofanywa kwa wakazi wa vijiji vya wilaya ya Magu, ambapo familia moja yenye zaidi ya watu kabla ya kula, hunawa maji kwenye bakuli moja kasha mara baada ya hapo mzee wa familia huyanywa maji hayo kama tiba ya kutanua kifua au humnywesha motto mchanga kwa makusudi hayo ya kumpanua kifua.

Takwimu za vyoo katika jiji la mwanza zinaonyesha kuwa vyoo bora ni asilimia 64%, vyoo duni ni asilimia 33% na nyumba ambazo hazina vyoo kabisa ni asilimia 3%, changamoto ya tatizo hilo ikitajwa kuwa ni pamoja na gharama kubwa ya vifaa vya ujenzi, umasikini na ufukara wa wananchi kutokana na kipato duni na kiwango cha uelewa,na hali ya miamba na baadhi ya maeneo kuwa na chemichemi nyingi hasa mabondeni.

Kwa upande wa matumizi ya vyoo kulingana na hali ya kijiografia na jinsi ujenzi holela milimani ulivyo, imegundulika kuwa siyo kwamba nyumba zote zilizoko sehemu za milima hazina vyoo bali taarifa sahihi ni kwamba vyoo vilivyopo maeneo hayo siyo bora na si vya kudumu.

Sambamba na maadhimisho hayo ambayo yamefanyika kwa kila halmashauri nchini huku mkoa wa Tanga yakifanyika kitaifa , halmashauri ya jiji la Mwanza kwa kushirikiana na PLAN INTERNATIONAL imefanya maonesho katika viwanja vya furahisha ya choo rahisi bora na cha kisasa kama darasa kwa wananchi.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm