Home » » MKANDARASI ANAYESAMBAZA KIFUSI PUNDE TU BAADA YA KUMWAGWA AWAFURAHISHA WATUMIAJI WA BARABARA MAKETE

MKANDARASI ANAYESAMBAZA KIFUSI PUNDE TU BAADA YA KUMWAGWA AWAFURAHISHA WATUMIAJI WA BARABARA MAKETE

Written By kitulofm on Wednesday, 13 November 2013 | Wednesday, November 13, 2013


Kazi ya kusambaza kifusi sekunde chache baada ya kumwagwa na lori barabarani ikiendelea kama ilivyonaswa na mwandishi wetu eneo la Mago wilayani Makete.
 
Wananchi wilayani Makete mkoani Njombe wamempongeza mkandarasi anayekarabati barabara kuu Makete - Njombe  katika kata ya Lupalilo kutokana na kitendo cha kulundika vifusi na kuvisambaza papo hapo

Inadaiwa kuwa mkandarasi huyo kuwenda akawa wa kwanza kufanya kitendo hicho wilayani hapa kwani wengi wamekuwa wakivilundika vifusi barabarani na kuviacha muda mrefu bila kuvisambaza hali inayosababisha kwero kwa watumiaji wa barabara hiyo

Mtandao huu umeshuhudia lori moja linapomwaga kifusi, greda linakisambaza kwanza na ndipo lori lingine linatakiwa kumwaga kifusi kingine

Hali hiyo imeonesha kuwafurahisha wengi hasa watumiaji wa barabara hiyo kwa kuwa hakuna usumbufu wa mlundikano wa vifusi kwa muda mrefu kama ilivyozoeleka kwenye suala zima la ujenzi wa barabara

barabara hiyo iliyopo chini ya TANRODS Njombe inaendelea na matengenezo ambapo kwa sasa wapo katika kata ya Lupalilo kuendelea na ujenzi huo
 
Na Edwin Moshi
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm