Home » » TAKWIMU ZAONESHA ONGEZEKO LA MAKUSANYO YA KODI NCHINI

TAKWIMU ZAONESHA ONGEZEKO LA MAKUSANYO YA KODI NCHINI

Written By kitulofm on Wednesday, 6 November 2013 | Wednesday, November 06, 2013


Takwimu zinaonyesha kuwa kumekuwa na ongezeko la makusanyo ya kodi ya ongezeko la thamani kwa asilimia 38 mwaka 2012/2013 kutokana na utumiaji wa mfumo mpya wa kutoa risiti kwa kutumia mashine za kielektronik na hivyo kuongeza kwa kiasi kikubwa mapato ya serikali.

Hayo yamebainishwa na meneja wa huduma kwa mlipa kodi Bwana Alllan Kiula wakati wa uzinduzi wa maonyesho ya siku ya mlipa kodi ambayo yanaendelea katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

Bwana Kiula amesema maonyesho ya mwaka huu yamekusanya wafanyabiashara mbalimbali kwa lengo la kuonyesha bidhaa zao pamoja na kuwapatia elimu juu ya utumiaji wa mashine hizo za kielektronic katika utoaji wa risiti kutokana na mauzo ya bidhaa ama huduma.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm