Home » » TRA MBEYA:AFANYABIASHARA WAKUBWA WANATUMIA MACHINGA KUANDAMANA

TRA MBEYA:AFANYABIASHARA WAKUBWA WANATUMIA MACHINGA KUANDAMANA

Written By kitulofm on Wednesday, 27 November 2013 | Wednesday, November 27, 2013




MENEJA wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Mbeya, Arnold Maimu amesema wanaogomea kutumia mashine za Kielotronik(EFD) ni wafanyabiashara wadogo ambao hata mashine hizo haziwahusu.
 
Aliyasema hayo jana wakati akijibu swali kutoka kwa Waziri wa Uchukuzi Dr. Harrison Mwakyembe alipotembelea banda ya maonesho la Mamlaka hiyo katika Maonesho ya Kimataifa ya kibiashara yanayofanyika katika viwanja vya ukumbi wa mikutano wa Mkapa uliopo Sokomatola Jijini Mbeya.
 
Maimu alisema wafanyabiashara wanaopaswa kutumia mashine hizo ni wake tu wenye uwezo wa kuingiza Milion 14 pamoja na wafanyabiashara wote wenye viwanda, biashara za jumla na rejareja, waliosajiliwa na ongezeko la thamani(VAT) na wale wote ambao wataamuliwa na Kamishina wa TRA kutumia mashine hizo.
 
Alisema mara nyingi wanaoonekana barabarani na kupinga matumizi ya mashine hizo ni wafanyabiashara ambao hawahusiki na wala hawajatajwa bali wanatumiwa na wafanyabiashara wakubwa.


Na Mbeya yetu
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm