Home » » UN YASEMA KESI DHIDI YA VIONGOZI WA KENYA ITAENDELEA

UN YASEMA KESI DHIDI YA VIONGOZI WA KENYA ITAENDELEA

Written By kitulofm on Sunday, 17 November 2013 | Sunday, November 17, 2013

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limetupilia mbali ombi la Umoja wa Afrika kutaka kuahirishwa kwa mwaka mmoja kesi dhidi ya Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta, na naibu wake William Ruto, katika mahakama ya ICC.

Wanachama wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa
Wanachama wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa

Ombi la serikali ya Kenya la kutaka kuahirishwa kwa kesi hiyo ya uhalifu halikukubalika baada ya wanachama 7 kati ya 15 waliopiga kura kukataa ombi hilo.

Nchi nane wanachama wa baraza hilo hazikushiriki katika zoezi hilo.
 Angalau kura takriban tisa zilihitajika ili kupita kwa azimio hilo lililotolewa na Umoja wa Afrika.
CHANZO dwkiswahili
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm