Home » » WAFUGAJI WAWATESA WAKULIMA

WAFUGAJI WAWATESA WAKULIMA

Written By kitulofm on Tuesday, 26 November 2013 | Tuesday, November 26, 2013


 KUNDI la wafugaji wakiwa na mifugo yao, wameendelea kuwatesa wakulima wa Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma  kwa kulisha mifugo yao kwenye mashamba ya mihogo, zao  ambalo ni tegemeo kubwa kwa wananchi wa wilaya hiyo.

Akizungumza kwa masikitiko, Allen Ngongole mkulima wa Kijiji  cha Ligera, alisema kuwa, mpaka sasa amepoteza ekari moja  ya shamba la mihogo kutokana na kuharibiwa na mifugo na kumfanya aishi porini kwa kulinda mashamba mengine  yasiharibiwe na mifugo hiyo.
            Zao aina ya Mtama
    Diwani wa Kata ya Ligera, Ally Ndauka alipohojiwa kwa njia  ya  simu kuhusu kuwepo kwa mifugo hiyo, alikiri kuwepo  kwa  mifugo hiyo, licha ya jitihada zake za kuwataka wafugaji hao kuondoka  katika maeneo yake na kuelekeza lawama kwa viongozi na  wananchi wa vijiji vya kata yake kuwakumbatia wafugaji hao.

Ndauka aliongeza kuwa, aliwasilisha taarifa ya kuwaondoa wafugaji katika kata yake kwenye  mkutano wa maendeleo ya  kata, pamoja na mambo mengine, aliwataka viongozi wa vijiji na  watendaji kushirikiana kuwaondoa wafugaji katika maeneo yao  na kupisha shughuli za kilimo, taarifa ambayo ilipingwa vikali na   wajumbe wa mkutano huo.

Akizungumza kwenye kikao cha Baraza la Madiwani hivi karibuni  Mkuu wa Wilaya hiyo, Abdul Lutavi aliwaagiza madiwani  kuhakikisha kwamba, wanawaondoa wafugaji hao katika maeneo  yao na kupisha shughuli za kilimo.

“Hakuna maeneo yaliyotengwa katika wilaya yangu kwa ajili ya  wafugaji pekee, hivyo kuendelea kubaki na kundi kubwa la wafugaji ni kukaribisha vurugu dhidi ya wakulima,“ alisema mkuu  wa wilaya huyo.

Baadhi ya wafugaji ambao hawakutaka kutaja majina yao, walisema kuwa, wapo katika maeneo hayo baada ya kukubaliwa na serikali za vijiji kuendelea na hsughuli zao.
Maeneo yaliyoathirika sana na wafugaji  hao katika Wilaya ya  Namtumbo ni Kata ya Mkongo, Ligera, Lusewa  na Magazine
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm