Home » » WANAMAKETE WATAKIWA KUSHIRIKIANA NA WADAU ILI KUTOKOMEZA UNYANYASI WA KIJINSIA

WANAMAKETE WATAKIWA KUSHIRIKIANA NA WADAU ILI KUTOKOMEZA UNYANYASI WA KIJINSIA

Written By kitulofm on Thursday, 21 November 2013 | Thursday, November 21, 2013

Jamii imetakiwa kushirikiana na wadau mbalimbali ili kutokomeza  suala la unyanyasaji wa kijinsia pamoja na ukatili dhidi ya wanawake.
Hayo yamesemwa  kwenye kipindi cha hazina ya mwanamke kinachorushwa na  kitulo fm kila siku ya jumapili saa mbili na 15 hadi saa tatu na 15 usiku na mtangazaji Veronica Mtauka(Super mama)

               Mtangazaji Veronica Mtauka
katika kipindi hicho cha hazina ya mwanamke aliweza kuzungumza na Fatuma Himili kutoka dawati la jinsia  kituo cha polisi Makete ambapo msimamizi wake ni WP Fatuma Himili kwa kata ya iwawa amesema kuwa wao kama dawati la jinsia wanakutana na changamoto mbalimbali ikiwemo wanawake kushindwa kutoa ushirikiano wa kuweza kuwafikisha wanaotenda ukatili dhidi ya wanawake katika vyombo vya sheria kama mahakamani 

Hata hivyo alikuwepo Bi. Monica Hindi kuto katika shirika la pamoja tuwalee (ELCT) lililopo wilayani hapa na makazi yao makuu yapo katika kata ya Iwawa Makete mjini amesema kazi yao kubwa ni kutoa elimu kwa jamii ili kutokomeza ukatili zidi ya wanawake na watoto kuanzia vijiji hadi mjini. 
Na Veronica Mtauka
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm