RAIS wa kwanza wa Afrika Kusini na mpinga siasa za ubaguzi
wa rangi, Nelson Mandela amefariki nchini humo akiwa na umri wa miaka 95.
Taarifa za kifo chake zimetangazwa na rais wa nchi hiyo,
Jacob Zuma ambaye amesema Mandela amefariki majira ya saa 2.50 usiku wa
Alhamisi kwa saa za Afrika Kusini.
Mandela amekuwa akisumbuliwa na maradhi kwenye mapafu kwa
muda mrefu, alilazwa na baadaye kuruhusiwa kutoka hospitali ambapo mauti
yamemkuta akiwa nyumbani kwake mjini Pretoria.
Tayari viongozi mbalimbali duaniani wameshaanza kutuma
salamu za rambirambi kwa familia na taifa la Afrika Kusini.
Viongozi hao ni pamoja na Rais Barack Obama wa Marekani na
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Ban Ki-Moon.
0 comments:
Post a Comment