Home » » SHULE YA KWANZA WILAYANI MAKETE YA WANAFUNZI WA KIKE KUANZA JANUARI 2014

SHULE YA KWANZA WILAYANI MAKETE YA WANAFUNZI WA KIKE KUANZA JANUARI 2014

Written By kitulofm on Saturday, 7 December 2013 | Saturday, December 07, 2013

Picha na Edwin Moshi
              
Haya ni madarasa yakiwasubiri wanafunzi januari mwakani

 Ndg.Kinana katikati akizungumza,kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Makete Mh.Josephine Matiro

 
  Mifuko ya Saruji iliyotolewa hapo jana

Chama cha mapinduzi (CCM) makao Makuu kupitia kwa katibu wake mkuu ndugu Abrahamani Kinana kimeahidi kutoa mabati 200 kwaajili ya kukamilisha ujenzi wa bweni la kulala wanafunzi katika shule ya wasichana iliyoko katika kijiji cha Utweve  kata ya ukwama  wilani hapa 

 Ndg.Kinana ametoa ahadi hiyo wakati alipotembalea shule hiyo nakujionea nguvu za wananchi kwashikiana na viongozi wao kuendelea kujenga majengo ikiwemo bwena la kulala wanafunzi pia ndugu kinana amempongeza mkuu wa wilaya Maketeb Josophine matiro kwa kushilikiana vizuri na wananchi na hususani suara la kuchangia ujenzi huo 

Aidha mpaka sasa wananchi waishio kijijini hapo na wale walioko nje ya wilaya  kwa kushirikiana  na Halmashauri pamoja na TASAF wameweza kujenga vyumba vitatu vya madarasa,vyoo pamoja na nyumba moja ya kuishi  mwalimu ikiwa mpaka sasa wanaendelea na ujenzi wa bweni litakalo kamilika mapema ili kusaidi wanafunzi hao kuishi shuleni hapo

 Shule hiyo inatarajiwa kuanza januari mwakani na itakuwa ikipokea wanafunzi wa kike kutoka sehemu mbalimbali na ikiwa ni shule ya kwanza ya wasichana wilayani Makete

Na Riziki Manfred
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm