Home » » TAARIFA KAMILI KUHUSU MTOTO ALIYEBAKWA MAKETE

TAARIFA KAMILI KUHUSU MTOTO ALIYEBAKWA MAKETE

Written By kitulofm on Wednesday, 8 January 2014 | Wednesday, January 08, 2014

Kijana mwenye umri wa miaka 36 anaetambulika kwa jina la Frasic Pila mkazi wa Iwawa anashikiliwa na jeshi la polisi wilayani makete kwa kosa la kumteka nyara na kumbaka binti mwenye umri wa miaka kumi na tano jila limehifadhiwa.

Akizungumza na kitulo fm kwa niaba ya mkuu wa polisi wilaya ya makete  OCD ,mkuu wa upelelezi wilaya OC CID  bwana Gozbert komba amesema tukio hilo lilitokea siku ya tarehe tatu mwezi huu maeneo ya iwawa na wao walipata taarifa siku ya tarehe tano kutoka kwa bwana Erick Mahenge ambae ni mfanyabiashara wa hapa mjini.

Amesema kuwa walipata taarifa saa mbili usiku kutoka kwamsamalia mwema Bw.Erick Mahenge kuwa mtoto huyo alitekwa nyara tarehe tatu januari mwaka majira ya saa saba mchana hadi kukutwa siku ya tarehe tanosaa saba na nusu mchana ambapo aligundua kutekwa nyara kwa binti huyo ambaye ni mfanyakazi wake wa kazi za ndani

Hata hivyo amesema kuwa binti huyo alikutwa akiwaamefungwa kamba katikamiguu yake pamoja na mokono kwa kutumia kamba ya katani na alikutwa katika nyumba moja akiwa amefungiwa ambayo haishi mtu (pagalo) 

Mara baada ya polisi kupata taarifa hizo walianza mapema kufuatilia walipomkuta siku hiyo binti alieleza kwamba anasiku tatu hajaweza kugusa chakula aina yoyote,katika hali hiyo waliweza kumkamata mtuhumiwa kwani ndiye aliweza kutoa taarifa za mhalifu huyo

Hata hakuna taarifa zozote zilizokuwa zimetolewakuhusu kubakwa kwake kutoka kwa madaktari ambapo Bw.Komba amesema kuwa wanasubiri taarifa kutoka wahudumu wa Afya kuhusu uhakika wa kubwakwa kwa mtoto huyo japokuna dalili zote za kuonesha kubakwa kulingana na mazingira yanavyoonesha wazi kuwa kuna dalili za kubwakwa kwa mtoto huyo
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm