Home » » WALIMU SHULE ZA MSINGI KATA YA LUPALILO WILAYANI MAKETE WAAZIMIA KUONGEZA KIWANGO CHA UFAULU KWA WANAFUNZI WAO

WALIMU SHULE ZA MSINGI KATA YA LUPALILO WILAYANI MAKETE WAAZIMIA KUONGEZA KIWANGO CHA UFAULU KWA WANAFUNZI WAO

Written By kitulofm on Friday, 31 January 2014 | Friday, January 31, 2014



         Picha na Henrick Idawa
Baadhi ya walimu wakiwa katika picha ya pamoja katika kata ya Lupalilo wilayani hapa

Shule za msingi kata ya lupalilo wialayani makete zimefanya kikao cha cha walimu wote wa kata hiyo kwa kuweka malengo na mikakati ya uboreshaji wa taaluma na mazingira ya shule katika kata ya lupalilo mwaka 2014.kwa lengo la kuinua kiwango cha elimu katika kata hiyo kutoka aslimia 80% ya matokeo ya darasa la saba mwaka 2013 hadi wafikie asilimia 85% kwa mwaka huu 2014.Ikiwa watafuata malengo na mikakati waliojiwekea.

Akisoma malengo katibu wa elimu kata bw.Orgen Sanga amesema kwa mwaka 2013 walijiwekea malengo ya kufuta daraja ‘E’ Katika ufaulu wa mitiani wa kuhitimu elimu ya msingi na kuongeza kuwa mwaka huu 2014 wamejiwekea malengo ya kuhakikisha kiwango cha ufaulu kutoka asilimia 80% ya sasa mpak 85% ifikapo Disemba 2014,kuongeza ufaulu wa masomo katika madaraja ‘A’,’B’ na ‘C’ na kupunguza daraja ‘D’ .Pia kuendelea kutopata daraja ‘E’ ambalo wamekwisha lifuta tayari,kuhakikisha wanafunzi wote wa darasa la pili (2) na tatu (3) wanamudu ABC za elimu ya msingi,’”KUSOMA’ “KUANDIKA’’ NA ‘’KUHESABU”.(KKK)

BW.SANGA amesema kufuatia “BRN” wanahakikisha kuboresha michezo na mazingira ya shule na kuwa na miradi ya shule ili kuongeza kipato cha shule mf.upandaji miti,matunda kilimo cha pareto na mazao ya chakula,kuwajengea wanafunzi stadi za maisha ili kuweza wanafunzi kuyakabili mazingira yao na changamoto za maisha.shule zote kutoa chakula cha mchana na kuandaa mipango ya shule kwa kuzingatia vigezio vyza BRN Matokeo makubwa sasa na kuwatumia takwimu.

Katika malengo hao shule hizo zimejiwekea mikakati ya kuwezesha haya yote waliojiwekea kufikia malengo haya mwaka huu 2014.wamekubaliana kuwa na mikakati ifuatayo kuongeza muda wa ufundishaji wa kujitolea asubuhi kabla ya vipindi na jioni baada ya vipindi vya kila siku,kuwa na majaribio ya kila baada kumalizika mada,majaribioo ya mwezi na mihula kwa madarasa yote,kuwa na mitihani miwili ya kata kwa darasa la saba na darasa la nne mmoja,kuwepo na kumbukumbu za kitaaluma kwa kila shule kila shule kuwa na mpango wa jumla wa maendeleo na kufuatilia utekelezaji wake,kuwepo na mikutano ya wazazi(parents day)mwezi juni na November mwishoni mwa mwaka na kutoa huduma ya ushauri nasaha na elimu ya VVU na UKIMWI kwa wanafunzi wakila shule katika kata ya lupalilo

Katika kikao hicho kilicho anza na kutathimini hali ya ufaulu wa wanafunzi mwaka 2013 kujiunga kidato cha kwanza mwaka 2014,walimu wamelalamikia kutokuwepo kwa ushirikiano katia ya mzazi,mwanafuinzi na mwalimu katika kuinua elimu,mfumo wa matumizi ya vitabu ambapo kwa sasa wanatumia zaidi ya aina 5 za vitabu kama taasisi,oxford,twiga nk.utoro wa wanafunzi kuhudhuria masomo,kuacha kwa masomo wanafunzi wa kidato cha kwanza na pili kunachangia kushusha hamasa kwa walioko mashuleni wakisubili kuhitimu.

Walimu hao wameongeza kuwa upungufu wa walimu ukizingatia idadi kubwa afya zao sio nzuri hivyo kwa wenye afya kuwa na mzigo mkubwa wa vipindi vya masomo,baadhi ya watoto kuwa na tatizo la akili hawafundishiki (mtitindio wa ubongo) na wameshauri kuwepo kwa kitabu kimoja kwa taifa zima ili kuepusha kutofautiana kwa majibu kati ya shule na shule.


Hata hivyo mratibu wa elimu kata MEK amesema kwa sasa kuna somo ambalo mwalimu wa sayansi na maarifa ya jamii wanatakiwa kufundishi ambalo kwa sasa wanasubili mtaala uletwe kuidhinishwa hivyo walimu wakae wakijua,somo ambalo litahusika na majanga ya eneo husika na kuwafundisha namna ya kuepuka na kuzuia majanga hayo mfamo,magonjwa ya mulipuko,mafuriko nk.

Na Henrick Idawa
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm