Home » » AFRIKA YATAKA MATAIFA MAKUBWA KUSAIDIA KUKABILIANA NA MABADILIKO YA TABIA YA NCHI

AFRIKA YATAKA MATAIFA MAKUBWA KUSAIDIA KUKABILIANA NA MABADILIKO YA TABIA YA NCHI

Written By kitulofm on Wednesday, 20 November 2013 | Wednesday, November 20, 2013

Nchi za Kiafrika zimeyataka mataifa makubwa duniani kuwa na utashi wa kisiasa katika kutekeleza ahadi za misaada ya kifedha itakayoziwezesha nchi zinazoendelea kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.
 
Akihutubia katika mkutano wa 19 wa umoja wa mataifa kuhusu mabadiliko ya tabia nchi mjini warsaw nchini poland, rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya marais wa afrika kuhusu mabadiliko ya tabia nchi mh jakaya kikwete,amesema pamoja na kuwa bara la afrika linazalisha kiasi kidogo cha hewa ukaa bara hilo limekuwa ni muathirika mkuu wa athari zitokanazo na mabadiliko ya tabia nchi hivyo ni budi nchi tajiri kulihakikishia bara la afrika vyanzo vya uhakika na endevu vya fedha,teknolojia pamoja na ujuzi wa kukabiliana na athari hizo.
 
Aidha rais kikwete amesema kuwa ni matarajio ya nchi za kiafrika kuwa mkutano wa poland utatoka na maamuzi ya msingi ikiwa ni pamoja na kuweka  utaratibu wa kushughulikia hasara na athari zitokanazo na mabadiliko ya tabaia nchi.
 
Kwa upande katibu mkuu wa umoja wa mataifa bwana ban ki moon amesema maafa yanayotokea hivi sasa katika maeneo mbalimbali ya dunia akitolea mfano maafa ya hivi karibuni nchini ufilipino ni matokeo ya athari za mabadiliko ya tabia nchi na kuongeza kuwa jitihada za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia ya nchi ni ndogo ikilinganishwa na athari ambazo dunia imeanza kuzishuhudia  na hivyo nguvu za ziada zinahitajika.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm