Home » » WACHINA MATATANI KWA KUDAIWA KUKAMATWA NA KIGANJA CHA BINADAMU

WACHINA MATATANI KWA KUDAIWA KUKAMATWA NA KIGANJA CHA BINADAMU

Written By kitulofm on Wednesday, 20 November 2013 | Wednesday, November 20, 2013

Watu wawili raia wa China ambao ni viongozi wa kiwanda cha Urafiki plastick kinachotengeneza mifuko ya aina mbalimbali eneo la Mabibo jijini Dar es Salaam,wameshikiliwa na jeshi la polisi kwa kudaiwa kufukia kiganja cha mkono wa mfanyakazi wao uliokatwa na  mashine za kiwanda hicho siku ya Jumapili usiku. 
 
ITV ilifika katika eneo la Mabibo jijini Dar es Salaam pembezoni mwa kiwanda cha urafiki plastick na kukuta watu wakiwa wanashangaa tukio la kufukiwa kwa kiganja hicho,ambapo ndugu wa bwana Jumanne Rashid ambaye amedaiwa kuwa ni mfanyakazi wa kiwanda hicho,wamesema ndugu yao alikatwa na mashine katika kiwanda hicho siku ya Jumapili usiku na wamiliki wa kiwanda hicho walipoulizwa wakadai mkono wa kijana huyo ilisagika kabisa hali iliyosababisha kijana huyo bwana Jumanne Rashid kulazwa katika hospitali ya taifa ya Muhimbili mpaka sasa.
 
Jitihada za ITV kuzungumza na raia hao wa China kuhusu tukio hilo ziligonga mwamba baada ya raia hao wa kigeni kudai kutokuwa na uwezo wa kuzungumza kiswahili wala kiingereza na hivyo kushikiliwa na maafisa wa polisi kisha kuondoka na kiganja hicho,ambapo ili kupata taarifa za hospitali ya taifa ya Muhimbili alikolazwa kijana aliyekatwa mkono zilishindikana baada ya afisa uhusiano wa hospitali hiyo bwana Aminieli Eligaesha kutopokea simu akidai yupo katika mkutano huku mkurugenzi mtendaji wa hospitali hiyo dakta  Marina Njelekela alipopigiwa simu alijibu yupo safarini nchini Marekani huku kamanda wa polisi mkoa wa Kipolisi Kinondoni ACP Camilius Wambura amethibitisha kukamatwa kwa kiganja hicho na kusema tayari kijana aliyekatwa mkono katika kiwanda hicho amehojiwa katika hospitali ya Muhimbili na wafanyakazi wa kiwanda hicho
CHANZO:ITV
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm