Home » » JELA MAISHA KWA KUMLAWITI MTOTO

JELA MAISHA KWA KUMLAWITI MTOTO

Written By kitulofm on Friday, 29 November 2013 | Friday, November 29, 2013

MAHAKAMA ya Wilaya ya Mpanda,  Mkoa wa Katavi  imemhukumu kifungo cha maisha jela mkazi wa Kijiji cha Mwese, Leonald William (19),  baada ya kupatikana na hatia ya  kumlawiti mtoto wa kiume  mwenye umri wa miaka saba ambaye jina lake limehifadhiwa. 
 
Hukumu hiyo ilitolewa jana na Hakimu   Mkazi  Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Mpanda, Chiganga  Ntengwa,  baada ya mahakama kumtia hatiani kwa kosa hilo.

Katika kesi hiyo ambayo ilikuwa na washitakiwa wawili,  mshitakiwa mwingine,  Ezekia   Yohane, mwenye umri wa miaka kumi na saba alihukumiwa adhabu ya viboko vinne  kutokana na umri wake kuwa mdogo.

Washitakiwa hao walidaiwa kutenda kosa la kumlawiti mtoto huyo  Julai 31, mwaka huu, majira ya saa mbili usiku nyumbani kwao mtoto huyo, ambapo washitakiwa hao walikuwa wameajiriwa  kufanya kazi ya kuchunga mifugo ya baba mzazi wa mtoto huyo.

 Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Chiganga alisema baada ya kusikiliza mwenendo  mzima wa kesi  mahakama  imewaona washitakiwa wana hatia.  

Washitakiwa kabla ya kusomewa hukumu  walipewa nafasi ya kujitetea   ambapo waliiomba Mahakama iwaachie huru  kutokana  na kile walichodai  kuwa walisingiziwa kosa hilo na baba wa mtoto huyo kwa kuwa walikuwa wakimdai pesa  za mishahara za muda mrefu. 

Baada ya maombi hayo, Mwendesha Mashitaka  Mkaguzi Msaidizi  wa Polisi, Ally Mbwijo,  alipinga vikali  maombi hayo  na kuiomba mahakama itoe adhabu kali kwa washitakiwa.
CHANZO:Tanzania Daima
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm