Home » » KINANA AITAKA SERIKALI KUWAONDOLEA VIKWAZO WANANCHI KATIKA SHUGHULI ZAO ZA KIMAENDELEO

KINANA AITAKA SERIKALI KUWAONDOLEA VIKWAZO WANANCHI KATIKA SHUGHULI ZAO ZA KIMAENDELEO

Written By kitulofm on Friday, 29 November 2013 | Friday, November 29, 2013

Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, akihutubia maelfu ya wananchi katika Uwanja wa Shule ya Msingi Mwaka, mjini Tunduma, wilayani Momba, jioni hii, Nov 28, 2013,Kinana ameitaka Serikali kupunguza ama kuwaondolea vikwazo  wananchi katika suala zima la kujiletea maendeo yao,pia ameongoza kuwa Viongozi wawasikilize Wananchi badala ya kuka maofisni na semina kila wakati ambazo hazina tija yoyote kwa wananchi,Ndugu Kinana na ujumbe wake yupo katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM, kusikiliza kero za wananchi na kuzungumza nao njia ya kuzitatua, katika mkoa wa Mbeya.

 
Sehemu ya umati wa watu waliofurika kwenye mkutano huo wa hadhara wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana ambaye aliwakonga nyoyo wakazi wa eneo hilo wakiwemo wapinzani kwa kusema kuwa hatakuwa tayari kuwavumilia viongozi wanaoshindwa kutatua kero za wananchi,waliojawa na umangimeza na urasimu.
 Katibu wa NEC, Siasa na Uhisiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro (katikati mwenye  miwani) akiserebuka na wananchi kwenye mkutano, Uwanja wa shule ya  Mwaka, Tunduma jana
 
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akihutubia katika mkutano mkubwa wa hadhara uliohudhuriwa na maelfu ya wananchi katika uwanja wa shule ya msingi Mwaka mjini Tunduma wilayani Momba mkoani Mbeya
  Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha Rose Migiro, akihutubia katika mkutano huo,ambapo alisisitiza kuweka kipaumbele cha elimu kwa watoto wa kike pamoja kupiga vita unyanyasaji wa wanawake na watoto.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm