Home » » MTU MMOJA AUWAWA KWA KUFUKIWA NA KIFUSI MKAZI WA IVALALILA WILAYANI MAKETE

MTU MMOJA AUWAWA KWA KUFUKIWA NA KIFUSI MKAZI WA IVALALILA WILAYANI MAKETE

Written By kitulofm on Friday, 8 November 2013 | Friday, November 08, 2013

Mtu mmoja ambaye ni mkazi wa kijiji cha Ivalalia kata ya Iwawa wilayani Makete amefariki dunia baada ya kudondokewa na kifusi cha mchanga wakati akichimba mchanga

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Mkuu wa upelezi wilayani Makete Bw.Gozbert Komba amemtaja mkazi huyo kuwa ni Daudi Ilomo (42)amesema kuwa amefariki dunia wakati akichimba mchanga kijijini hapo

Aidha ameongeza kuwa marehemu ameongeza kuwa marehemu amekutwa akiwa amevunjika mguu mara mbili,pia alitokwa na damu puani na masikioni baada ya kifusi hicho kumbana katika mwili wake hasa kifuani

Hata hivyo marehemu wakati wa uhai wake na kwa mara ya mwisho alikuwa na Bw.Polito ilomo

Pia ametoa wito kwa wananchi  wote kuwa makini pindi wanapokuwa katika maeneo wanaojua kuwa ni hatarishi kwao kuwa katika makundi ili kusaidiana na kujiepusha katika majanga kama ya aina hiyo
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm