Home » » PINDA:AFRIKA IRIDHIE MAHAKAMA HAKI ZA BINADAMU

PINDA:AFRIKA IRIDHIE MAHAKAMA HAKI ZA BINADAMU

Written By kitulofm on Wednesday, 20 November 2013 | Wednesday, November 20, 2013

Mizengo PindaWAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda, amezishauri nchi zote za Afrika kuridhia mikataba ya uanzishwaji wa Mahakama ya Haki za Binadamu ya Afrika iliyopo mjini Arusha ili kutoa fursa kwa makundi, taasisi binafsi na raia kuitumia mahakama hiyo pindi ukiukwaji wa haki za binadamu unapofanywa katika nchi zao.

Pinda alitoa wito huo mjini hapa jana alipofungua semina ya siku tatu ya wakuu wa vyombo vya sheria na majaji kutoka nchi wanachama wa Afrika na taasisi za kimataifa za kisheria iliyoandaliwa na Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu.

Mpaka sasa ni nchi 26 barani Afrika zilizoridhia uanzishwaji wa mahakama hiyo huku nchi saba zikitoa fursa kwa taasisi binafsi na hata mtu mmoja mmoja kuwa na uwezo wa kufungua shauri katika mahakama hiyo ikiwemo Tanzania.

Alisema ni vema nchi zote zikaridhia ili kutoa wigo mpana wa si tu wa demokrasia katika nchi zao, bali kutoa fursa kwa raia wa kawaida kuwa na haki ya kushtaki katika mahakama hiyo kama nchi yake na mahakama ya  nchi yake imekiuka moja ya haki za binadamu.

“Sisi kama Tanzania tumeridhia mkataba huo na kwa kiasi kikubwa tunautekeleza kwa vitendo ndiyo maana hata waziri mkuu alipotoa matamko ambayo baadhi ya asasi binafsi za kisheria zikadhani amekiuka moja ya haki za binadamu wakaamua kufungua jalada mahakamani na kesi inaendelea,” alisema Pinda.
Akieleza malengo ya semina hiyo, Jaji Mkuu wa Tanzania, Othmani Chande, alisema majaji na wakuu wa mahakama mbalimbali Afrika na baadhi ya nchi nyingine walioshiriki wanataka kushauriana jinsi ya kuweza kuwa na tafsiri iliyo sawa juu ya haki za binadamu.

Alisema hivi sasa kila nchi inalinda haki za binadamu kupitia katiba zao, lakini wakaona ni bora wakashirikishana kuwa na tafsiri moja juu ya haki za binadamu katika mataifa yote ya Afrika.

Akizungumzia suala la viongozi wa Afrika kupelekwa katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC), alisema tayari nchi za Afrika zimeomba mkataba wa Roma upitiwe upya kutoa nafasi kwa mahakama za kanda za Afrika kushughulikia kesi hizo.

Rais wa mahakama hiyo, Jaji Sophia Akuffo, alisema nchi za Afrika haziwezi kuwa na amani ya kudumu kama suala la haki za binadamu halitazingatiwa.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm