Home » » WANANCHI WA KIJIJI CHA UTWEVE,MASISIWE NA USAGATIKWA MAKETE WAENDELEA NA UJENZI WA BARABARA

WANANCHI WA KIJIJI CHA UTWEVE,MASISIWE NA USAGATIKWA MAKETE WAENDELEA NA UJENZI WA BARABARA

Written By kitulofm on Wednesday, 20 November 2013 | Wednesday, November 20, 2013




Wananchi wa kijiji cha Utweve,Masisiwe kata ya Ukwama na Usagatikwa kata ya Tandala wilayani Makete wanaendelea na ujenzi wa kuunganisha barabara kati ya vijiji hivyo ulioanza mwaka 2011

Akizungumza na kitulo fm Mwenyekiti wa kijiji hicho Bw.Lauten Enock Sanga amesema kuwa shirika la TASAPH ndilo lililowataka wananchi wa vijiji hivyo kuibua mradi wowote na wananchi hao wakaamua kutengeneza barabara itakayo viunganisha vijiji hivyo


Amesema mradi huo gharama zote ni nguvu za shirika hilo ambapo walianza ujenzi wa barabara hiyo mwaka 2011 ikiwa hadi sasa mkakati wa ukamilishaji wa kuweka makaravati katika barabara hiyo unaendelea

Hata hivyo amelishukuru shirika la TASAPH kwa jitihada hizo kwani itasaidia hata kukuza kiwango cha uuzaji wa mazao na kurahisisha usafiri kati ya vijiji jirani hivyo na kuongeza kuwa wananchi wameupokea kwa mikono miwili mradi huo ambapo pia umetoa ajira kwa wakazi wa vijiji kwa kufanya kazi za kukwetua,kufenya nyasi pamoja na kuchimba barabara hiyo.

Na Furahisha Nundu

Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm