Home » » WATEJA WA MKAA MAKETE WALALAMIKIWA NA WAUZAJI WA MKAA

WATEJA WA MKAA MAKETE WALALAMIKIWA NA WAUZAJI WA MKAA

Written By kitulofm on Wednesday, 6 November 2013 | Wednesday, November 06, 2013

MAKETE

Wafanyabiashara wa mkaa Wilayani Makete mkoani Njombe Wanakabiliwa na changamoto kubwa ya wateja wa mkaa huo kuwa wasumbufu pindi wanunuapo mkaa

Wameyasema hayo mapema hii leo walipo kuwa wakizungumza na kitulo fm eneo la sokoni Makete mjini ambapo wauzaji hao wanafanyia biashara hiyo

 Wamesema kuwa wanakerwa sana na tabia ya wateja walio wengi kuambiwa wabebe mkaa huo kwa umbali mrefu hadi majumbani kwao pasipo kupewa fedha yoyote mbali na fedha ya mkaa

Wafanyabiashara hao wamesema kuwa fedha ya kununulia mkaa ni vema ingelikuwa tofauti na fedha ya kubebea mkaa huo.

Aidha wafanyabiashara hao wamezungumzia kuhusu kushuka kwa bei ya mkaa kutoka Sh.10,000-5000 kwa gunia
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm