Home » » DK.SHEIN AITAKA SUZA KUELEKEZA MIKAKATI YAKE KWA MAENDELEO YA NCHI

DK.SHEIN AITAKA SUZA KUELEKEZA MIKAKATI YAKE KWA MAENDELEO YA NCHI

Written By kitulofm on Sunday, 29 December 2013 | Sunday, December 29, 2013


Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein ameutaka uongozi wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) kuhakikisha kuwa upanuzi wa mitaala, ufundishaji na tafiti zinazofanywa na chuo hicho zinaelekezwa katika kutoa michango na rai zitakazochangia na kurahisisha utekelezaji wa mipango ya maendeleo ya nchi.
 
Akizungumza wakati wa mahafali ya tisa ya Chuo Kikuu hicho yaliyofanyika jana huko Tunguu, mara baada ya kuwatunuku vyeti, stashahada na shahada wahitimu 763, Dk. Shein amesema ni jukumu la vyuo vikuu hasa vya serikali kutoa taaluma inayolenga kurahisisha utekelezaji wa mipango ya maendeleo taifa na jamii kwa ujumla.
 
Alisema zitihada zinazofanywa na chuo za kukuza elimu zitakuwa na manufaa zaidi endapo elimu itakayotolewa italiongoza Taifa na itatumika kurahisisha maisha na kuimarisha maendeleo kwa kusaidia utekelezaji wa Dira ya Maendeleo 2020, MKUZA II, Malengo ya Milenia na Ilani ya Uchaguzi ya CCM.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm