Home » » WANANCHI IHANGA WAAMUA KUTENGENEZA BARABARA ZA MITAA

WANANCHI IHANGA WAAMUA KUTENGENEZA BARABARA ZA MITAA

Written By kitulofm on Wednesday, 25 December 2013 | Wednesday, December 25, 2013

Wananchi wa kijiji cha Ihanga kata ya Ukwama wilayani Makete wameamua kutengeneza barabara za mitaa ili kurahisisha tatizo la mawasiliano ktk miundombinu

Kijiji hicho chenye zaidi ya wakazi 500 tokea kuanza kwake hakijawahi kuwa na barabara za mitaa hivyo wameamua kuanza usembuaji wa barabara hizo,wazo hilo lilikuja mara baada ya kuona kupata shida linapotokea tatizo la msiba wakati wa kwenda mazikoni ndipo waliamua watengeneze barabara ili ziwarahishie kupita

Kitulo imezungumza na Afisa Mtendaji wa kijiji hicho Bw.Bensony Mbilinyi ameelezea changamoto iliyokuwepo baada ya kutokuwa na miundombinu ya barabara hizo hivyo amewaomba wananchi kujitokeza kwa wingi pindi wanapotangaza siku na muda wa kwenda kushirikiana ktk kazi hiyo

Kijiji hicho chenye jumla ya vitongoji 6 kimeonekana kuwa na ushirikiano mkubwa kati ya kitongoji na kitongoji hata hivyo kila kitongoji wanasembua barabara kutoka kitongoji chao hadi kufikia kitongoji kingine 
 Na Furahisha Nundu
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm