Home » » MAKETE WAHAKIKISHIWA UMEME&BARABARA KUSHUGHULIKIWA MAPEMA MWAKA HUU

MAKETE WAHAKIKISHIWA UMEME&BARABARA KUSHUGHULIKIWA MAPEMA MWAKA HUU

Written By kitulofm on Wednesday, 8 January 2014 | Wednesday, January 08, 2014

 






















M/kiti wa Halmashauri ya wilaya ya Makete Mh.Daniel Okoka
Wananchi wilayani Makete wameeleza changamoto mbalimbali kwa Mh.Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Makete Bw.Daniel Okoka ikiwemo kero ya Umeme kutoka Makete-Tandala,Miundombinu ya barabara,Elimu,Afya pamoja na Redio kitulo fm kutofika katika baadhi ya maeneo wilayani Hapa

Kero hizo zimetolewa na wananchi usiku wa kuamkia leo katika kipindi cha Maalumu cha Twanga swali hapa kitulo fm kilichodhaminiwa na Gazeti la Daraja lililopo Mkoani Njombe kipindi hicho kiliochofanywa kuanzia saa 1:15 usiku hadi saa 3:20 usiku hapa kitulo fm hapo jana

Kuhusu suala la Umeme kwa wananchi wa Tandala hasa kitongoji cha Kilovoko amesema kuwa nguzo zimesimama pamoja na nyaya,transfoma zimefungwa hivyo kinachosubiriwa ni mchakato wa kuunganisha umeme katika Gredi ya Taifa kutoka Mbeya uliopo Makete mjini na sasa zoezi hilo lipo ukingoni hivyo amewaomba wananchi kuwa na subira katika hili kwani Mkandarasi anaendelea na kazi

Hata hivyo akijibu suala la Barabara ya Lupila ameelezea mengi na kusema kuwa zaidi ya kiasi cha sh.milioni 27 katika fedha zilizotengwa za matengenezo ya barabara kwani hata hivyo fedha hizo bado hazijatolewa hivyo mara baada ya kutolewa mapema ukarabati wa barabara hiyo utaanza mapema

Kwa upande wa Kuboresha masafa ya Redio Mh.Okoka amesema kuwa kuna mabadiliko mengi yaliyofanywa ikiwemo kubadilisha uongozi wa Redio pamoja na vipindi vyake kuimarishwa,wamefanya jitihada za kuunda bodi ya Redio ambayo wanauhakika itasimamia kiuhakika shughuli zote na kuweza kuongeza chachu ya kukua kwa Redio hata hivyo amesema kuwa kuna Mradi wa UNISEF kwa kushirikiana na Redio Clauds Fm walianza kutoa msaada ili kuboresha hayo yote katika redio lakini kuna watu wamehujumu kwa upande wa fedha hivyo kusababisha kukwama hivyo anataka andiko maalumu kuhusu fedha hizo kwa watu waliohusika mara moja.


Na Furahisha Nundu
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm