Home » » HABARI | UJENZI WA KITUO CHA MABASI MANISPAA YA IRINGA UMESTISHWA.

HABARI | UJENZI WA KITUO CHA MABASI MANISPAA YA IRINGA UMESTISHWA.

Written By kitulofm on Tuesday, 25 February 2014 | Tuesday, February 25, 2014

 IRINGA

Ujenzi wa kituo cha Mabasi cha Igumbilo Manispaa ya Iringa umesitishwa baada ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Mazingira, Dk. Binilith Mahenge kuamuru tathimini ya athari ya mazingira ifanywe upya.

Waziri amefikia uamuzi huo baada ya kutembelea eneo la ujenzi wa kituo hicho kufuatia kupata malalamiko juu ya athari za kujenga kituo hicho kutoka kwa Wizara ya maji, Mkoa wa Iringa na Mamlaka ya maji safi na maji taka mjini Iringa (IRUWASA) kuwa ujenzi wa kituo hicho utaathiri afya za watumiaji wa maji wa Iringa.

Dr mahenge amesema ni  vyema Halmashauri ya Manispaa hiyo kusitisha shughuli zote za kuendeleza eneo hilo kusubiri maamuzi ya serikali.

Aidha ameongeza kuwa hawezi kulitolea uamuzi suala la ujenzi wa kituo hicho bila kuwashirikisha wataalamu na kumuagiza Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Bonaventura Baya kurudia kufanya tathimini upya ili kubaini tatizo lilopo pamoja na madhara yatakayojitokeza.

Naye Mkurugenzi wa NEMC , Baya anasema watafanya tathimini hiyo kwa muda wa wiki mbili na kuhakikisha kuwa majibu yatakuwa tayari ili kuweza kusaidia maamuzi kutolewa mapema kwa kufuata ushauri wa wadau mbalimbali juu ya ujenzi huo wa stendi ya Igumbilo.

Kwa upande wake Mstahiki Meya wa Manispaa ya Iringa, Amani Mwamwindi amesema ni vyema haki ikatendeka ili jambo hilo lisichukuliwe na kuonekana ni suala lenye maslahi ya kisiasa kwa baadhi ya wanasiasa.

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dk. Christine Ishengoma amesema kuwa kinachotakiwa ni kufanya subira ya matokeo ya NEMC na maamuzi ya serikali na kuwa kujenga au kutojenga kituo hicho ni maamuzi yatakayotolewa na serikali.

Akitoa Taarifa kwa waziri, Katibu Tawala wa Mkoa, Wamoja Ayubu anasema kuwa ujenzi wa kituo hicho ni mzuri na unadhana ya kuboresha miundombinu ya Manispaa ya Iringa, kukuza uchumi pamoja na kuvutia wawekezaji.

Aidha Wamoja anasema maji ya mto ruaha ni chanzo muhimu cha maji kwa wakazi wa Manispaa ya Iringa na kuwa IRUWASA imewekeza zaidi ya Sh70 Bilioni kwenye mto huo ili kuwapatia wananchi maji safi.

Iruwasa wanadai kuwa ujenzi wa kituo hicho utaendanana na shughuli za kibiashara na gereji jambo litakaloathiri maji kwa kuwa chujio zilizofungwa hazina uwezo wa kuchuja tqaka kemikali.

Wamoja alisema kuwa ujenzi huo endapo utatiririsha maji machafu taka ngumu na kemikali itaathiri maji ya mto Ruaha na pia itasababisha wakazi wa Iringa kuwa hatarini kutokana na kunywa maji yasiyo salama. 
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm