Kazi ya kutafuta mabaki ya miili ya
raia wawili wa Ufaransa waliouwawa kwa kukatwakatwa kwa mapanga na
kutupwa katika kisima huko Matemwe katika Mkoa wa Kaskazini,
imekamilika, imefahamika.
Akizungumza na Mwananchi jana, Mkuu wa Mkoa wa
Kaskazini Unguja, Pembe Juma Khamis, alisema kazi ya kufukuwa kisima
hicho ilikamilika saa 9:00 alasiri ya juzi.
Alisema kazi hiyo ilifanywa kwa ushirikiano wa Kikosi cha Zimamoto na Uokozi ,Polisi na wananchi wa shehiya hiyo.
0 comments:
Post a Comment