IRINGA
Wakazi
wa jimbo la kalenga,wilaya ya Iringa vijijini,mkoani
Iringa wameombwa kuwa watulivu na kuendelea kuilinda amani iliyopo
katika kipindi hiki cha kampeni zinzoendelea na kuelekea uchaguzi wa
mbunge jimbo humo.
Katibu
mkuu wa chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA,Dr Willbrod
Slaa,amesema hayo wakati alipokuwa akifungua kampeni za ubunge za chama
hicho,February 22 zilizofanyika kwenye viwanja vya ngome ya Mkwawa kata
ya Kalenga,mwenyekiti wa chama cha mapinduzi CCM mkoani iringa.
Dkt.Slaa ameongeza kuwa mchakato wa kumpata mgombea ndani ya chama hicho ulifanyika ambapo mgombea
alipatikana baada ya kupigiwa kura na wajumbe
zaidi ya 400,lakini alishindwa kutetea nafasi hiyo katika kura za
wagombea wenyewe wapatao 13 na nafasi yake kuchukuliwa na Grace Tendega.
Aidha
Dr Slaa ameongeza kuwa CHADEMA kitaendelea kusimamia suala la kuto
ongezwa kwa posho ya sh.lakitatu inayodaiwa ni ndogo na baadhi ya
wajumbe wa bunge la katiba ambapo mwenyekiti wa chama hicho yupo kwenye
kamati tendaji ya kujadili suala hilo.
Naye mgombea wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Bi. Grace Tendega amesema wananchi ndio wenye
jukumu la kumpima na kumchagua ambapo yeye atashughulikia changamoto za jimbo hilo ikiwa ni pamoja na ukosefu na ucheleweshwaji wa pembejeo.
Kwa
upande wa Chama Cha Mapinduzi wanaendelea na mikutano kwa maandalizi ya
ufunguzi rasmi wa kampeni hizo ambazo wanatarajia kufungua februari 27
mwaka huu.
Akizungumza
na wananchi wa kijiji cha Ugwachanya kata ya Mseke jimboni humo
februari 23,mwaka huu,Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa Bi.Jesca
Msambatavangu,amesema vijana na wakazi wa jimbo hilo wasikubali kuingia
kwenye vurugu zinazo
fanywa na baadhi ya vyama vya siasa,na kuwataka watambue thamani ya
amani iliopo kwa sasa hapa nchi.
Naye
mgombea wa nafasi hiyo kupitia CCM Bw.Godfley Mgimwa,amesema
ataakikisha kuwa huduma za jamii zinaboreshwa ikiwa ujenzi wa
zahanati,pamoja na shule pia wakazi wa kalenga
watambue kuwa yeye ni mtanzania halali,na si kama ilivyo elezwa awali na
chadema na amewataka watanzaia waishi kwa amani na kuto kubaguana.
Kampeni hizo zinatarajiwa kuhitimishwa machi 16,mwaka huu,ambapo kwa mujibu wa ratiba ya Chadema kitakuwa kimefanya
kampeni 760 kabla ya wananchi kupiga kura machi 16,mwaka huu.
-ENDS-
0 comments:
Post a Comment