Home » » WANAMAKETE WATAKIWA KUPENDA KUJISOMEA VITABU MARA KWA MARA

WANAMAKETE WATAKIWA KUPENDA KUJISOMEA VITABU MARA KWA MARA

Written By kitulofm on Saturday, 1 February 2014 | Saturday, February 01, 2014

 Kushoto ni Askofu mstafu wa Dayosisi ya kusini Kati Dkt. Solomon Swalo na Kulia ni Askofu wa KKKT wilayani Makete
 Kundi la wachungaji wakielekea Kanisani
 Kushoto ni Mwenyekiti wa Halmashauri wilaya Makete,Katikati ni Mkuu wa wilaya ya Makete na Kulia ni aliyekuwa Msaidizi wa askofu msataafu Mch.Manyewa
  Wanakwaya wakiimba nyimbo 
Kwa habari,picha zote na Edwin Moshi Makete

Wananchi wilayani Makete Mkoani Njombe wametakiwa kujijengea utaratibu wa Kujisomea Vitabu Mbalimbali  kwani ni Njia Moja wapo yakuongeza Maarifa.

Kauli hiyo imetolewa na Askofu mstafu wa Dayosisi ya kusini Kati Dkt. Solomon Swalo katika Tafrija ya kumpongeza baada ya kutunukiwa shahada ya Uzamivu (PHD) iliyofanyika jana Bulongwa wilayani hapa

Dkt. Swalo ambaye pia ni mwandishi mahili wa vitabu amesema amekuwa akiandika vitabu mbalimbali kwa ajili ya kuweka kumbukumbu ya vizazi vilivyopo na vijavyo lakini hakuna wasomaji wa vitabu hivyo.

Akizungumza kwa niaba ya Serikali Mkuu wa Wilaya ya Makete Josephine Matiro Amesikitishwa na tabia ya Baadhi ya watu ya kuto kupenda kusoma Vitabu na kuwataka wananchi kuanza kujisomea.

Matiro amesema kuwa serikali ipo pamoja na kanisa ili kuleta maendeleo Hivyo anaimani mchango wa Askofu Mstaafu Dk. Swalo bado Unahitajika sana katika Jamii.

Katika Hatua nyingine kanisa limempa Hati ya Jengo Askofu Dk Swalo kwa ajili ya kuuzia Vitabu lililopo Eneo la Namanga Bulongwa.


Tukio Hilo la Kumpongeza Dk Swalo limehudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Serikali,kanisa pamoja na wananchi.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm