Home » » APANDISHWA KIZIMBANI KWA KUMPA MWANAFUNZI MIMBA WILAYANI MAKETE

APANDISHWA KIZIMBANI KWA KUMPA MWANAFUNZI MIMBA WILAYANI MAKETE

Written By kitulofm on Tuesday, 25 March 2014 | Tuesday, March 25, 2014



Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Godfrey Sanga amepandishwa kizimbani mach 2014 katika mahakama ya wilaya Makete Mkoani Njombe kwa tuhuma ya kumpa mimba mwanafunzi.

Akielezea kutokea kwa  tukio hilo mwendesha mashtaka wa polisi Bw,gosbet komba mbele ya  hakim wa wilaya mh, j, s. obas amesema tukio hilo limetokea februali 2 mwaka huu majira ya saa moja usiku katika kata ya tandala.

Bw.Komba  amesema mtuhumiwa huyo amefanya tukio hilo la kumpa mimba mwanafunzi na kumsababishia kukatisha  masomo yake.

Hata hivyo mshtakiwa huyo amekana shitaka linalo mkabili na dhamana yake iko wazi kwa wadhamini wawili wa kuaminika na sh. Milioni moja kwa kila mmoja na mtuhumiwa huyo yuko nje kwa dhamana mpaka kesi yake itakapo tajwa tena aprili 04 mwaka huu.
Jina la mwanafunzi huyo limehifadhiwa,


Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm