Home » » IDARA YA ELIMU WILAYANI MAKETE NJOMBE YALALAMIKIWA

IDARA YA ELIMU WILAYANI MAKETE NJOMBE YALALAMIKIWA

Written By kitulofm on Thursday 17 April 2014 | Thursday, April 17, 2014



Baadhi ya walimu wakiwa katika picha ya pamoja 
             Picha na Furahisha Nundu
Uongozi wa shule ya Msingi Ibaga kata ya Mang’oto wilaya ya Makete Mkoani Njombe umeilalamikia serikali kutoangalia suala la ukuzaji wa taaluma katika shule hiyo

Akizungumza na Kitulo fm Mkuu wa shule hiyo Mwl.Ambonwilo Chengula amesema kuwa shule yake haijapokea walimu wa mazoezi kwa muda mfupi ilihali shule za jirani zimepata walimu hao

Shule hiyo inajumla ya walimu 8 ambapo mwalimu mmoja kati ya hao anasumbuliwa n a maradhi na mungine yupo masomoni hivyo kuna changamoto kubwa ya kuhakikisha kuna ukuaji wa taaluma shuleni hapo

Amesema Shule hiyo inazaidi ya wanafunzi 180 kiwango ambacho ni kikubwa ukilinganisha na walimu sita tu wanaofanya kazi kwa wakati huu pamoja na walimu wapywa waliopelekwa

Pia Mkuu huyo amesema kuwa tatizo hilo limechangiwa hasa na tatizo la ubovu wa miundombinu pamoja na kutokuwepo kwa mawasiliano ikiwa endapo serikali italitilia maanani suala la miundombinu na mawasiliano ni jambo ambalo litasaidia walimu kupatikana na kuongeza kiwango cha ukuaji wa elimu shuleni hapo
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm