Home » » WATOTO WAKIMBIZI WALIOPO KENYA WAANDIKA BARUA YA KUWAKUMBUA WAKIMBIZI WENZAO

WATOTO WAKIMBIZI WALIOPO KENYA WAANDIKA BARUA YA KUWAKUMBUA WAKIMBIZI WENZAO

Written By kitulofm on Thursday 17 April 2014 | Thursday, April 17, 2014

Vijana wakimbizi wanaoishi katika kambi kubwa zaidi ya wakimbizi duniani, nchini Kenya, Dadaab wamewatumia barua za kuwapa matumaini watoto wanaokumbwa na vita nchini Syria, ambao wamelazimika kutoroka vita na kukimbilia nchi jirani.

Wakimbizi hao wanaishi Dadaab Kaskazini mwa Kenya. Ni makao kwa wakimbizi 400,000 wengi wao waliotoroka vita, njaa na ukame nchini Somalia.
Vita hivyo vimekuwa vikiendelea kwa miaka 23 sasa.
Shirika la misaada la kimataifa la Care International, ambalo hutoa misaada kwa wakimbizi hao, liliandaa mpango wa kuandikiana barua kati ya watoto hao na wale wa Syria wanaoishi katika kambi ya wakimbizi ya Amman nchini Jordan.

Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm