Home » » WANANCHI WA KIJIJI CHA IDENDE MAKETE MKOANI NJOMBE WAKOSA MAJI KWA ZAIDI YA MWAKA HADI SASA

WANANCHI WA KIJIJI CHA IDENDE MAKETE MKOANI NJOMBE WAKOSA MAJI KWA ZAIDI YA MWAKA HADI SASA

Written By kitulofm on Tuesday 22 April 2014 | Tuesday, April 22, 2014

 
Wananchi wa kijiji cha Idende kata ya Bulongwa wilayani Makete Mkoani Njombe wameamua kuivunja kamati ya ya maji ya kijiji baada ya kukosa maji kwa zaidi ya mwaka mmoja hadi sasa

Katika hali ya vuta nikuvute iliyochukua muda mrefu wananchi wameamua kuivunja kamati ya maji kijijini hapo iliyokuwa na watu saba iliyokuwa ikiongozwa na mwenyekiti Bahati Sanga na kuunda kamati mpya yenye watu nane kwa kuzingatia jinsia mbele ya Mkutano wa Hadhara uliofanywa na wananchi zaidi ya 300

Maaumuzi hayo yamefanywa na wananchi wa kijiji hicho baada ya kuwepo malumbano yasiyotajwa kiini chake kati ya Fundi maji wa kijiji hicho na Kamati ya maji iliyonundwa kwa ajili ya kushughulikia huduma ya maji kijijini hapo inapatikana kwa muda wote

Naye Afisa Mtendaji wa kijiji hicho Bw.Elia Kyando amesema kuwa wananchi wameamua kuchukua uamuzi huo baada ya kuona kumekuwepo malumbano kati ya Fundi maji na kamati hiyo na kusababisha ukosefu wa maji ndani ya mwaka mzima hadi sasa

Bw.Jerald Tweve ambaye ni Fundi maji katika kijiji hicho amesema kuwa tatizo la wananchi hao kukosa maji ni Uchakavu wa Miundombinu ya maji iliyotokea katika kijiji cha jirani cha Imehe kata ya Bulongwa hivyo maboresho ya haraka yanahitajika ili kuhakikisha wananchi wanaipata huduma hiyo

Bw.Tweve Amewataka wananchi kuwa na subira na kusema kwamba atafanya jitihada zake kuhakikisha wananchi hao wanapata huduma ya maji ndani ya mwezi mmoja ujao
Na Furahisha Nundu
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm