Home » » ZOEZI LA UPIMAJI NA UGAWAJI WA VIWANJA KWA WAFANYABIASHARA WILAYANI MAKETE UMEKAMILIKA RASMI

ZOEZI LA UPIMAJI NA UGAWAJI WA VIWANJA KWA WAFANYABIASHARA WILAYANI MAKETE UMEKAMILIKA RASMI

Written By kitulofm on Tuesday, 12 November 2013 | Tuesday, November 12, 2013



Na Ergon Elly & Fadhil Lunati

MAKETE

Zoezi la Upimaji na Ugawaji wa Viwanja katika  eneo la Soko Kuu Makete kwa wafanyabiashara waliobomolewa Vibanda vyao kupisha ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami wilayani  Makete Mkoani Njombe limekamilika rasmi hii Leo kwa Wafanyabiashara na Kukabidhiwa Viwanja hivyo kwa ajili ya kuanza Rasmi Ujenzi Huo.

Hayo yamesemwa na Afisa Ardhi wilaya ya Makete Bw. Anikas Vilumba wakati alipokuwa akifanya Shughuli ya Upimaji wa Viwanja Hivyo kwa Wafanyabiashara na ameongeza kuwa Endapo wafanyabiashara watajitokeza katika eneo hilo la Viwanja watakabidhiwa kwaajili ya kuanza Rasmi kwa Ujenzi wa Vibanda vya Biashara kwa walio athirika na zoezi na bomoabomoa.

Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm