Katibu wa CCM
Mkoa wa Njombe Bwana Hosea Mpagike Akizungumzia Ratiba ya Ziara ya
Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndugu Abdurlahman Kinana na Msafara Wake Mkoani
Njombe.
Na Gabriel Kilamlya Njombe
Katibu Mkuu
wa Chama cha Mapinduzi CCM Taifa Abdurlahman Kinana Anatarijia Kuwasili
Mkoani Njombe leo Jioni Kwa Ziara ya Kikazi ya Siku Mbili Ikiwa ni
Muendelezo wa Ziara Yake ya Kutembelea Kukagua Miradi Mbalimbali ya
Maendeleo.Ujio wa Katibu Mkuu wa Chama Hicho Bwana Kinana Umelenga Kukagua Shughuli Mbalimbali Zinazofanywa na Vijana Katika Maeneo Mbalimbali Pamoja na Chama cha Mapinduzi CCM Ikiwa ni Pamoja na Kuhakikisha Serikali Inatekeleza Ilani ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2010/2015 Kama Inavyosema.
Akizungumzia Juu ya Ziara ya Kiongozi Huyo wa Kitaifa,Katibu wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Njombe Bwana Hosea Mpagike Amesema Kuwa Bwana Kinana Pia Ataongozana na Viongozi Mbalimbali wa Chama Akiwemo Mbunge Mteule Dokta Asha Rose Migiro Pamoja na Katibu Mwenezi wa CCM Taifa Ndugu Nape Mnauye.
Bwana Mpagike
Amesema Kuwa Kinana Ataanzia Ziara Yake Wilayani Makete Katika Mkoa wa
Njombe Ambapo Disemba 6 Mwaka Huu Atakuwa Wilayani Hapa Katika Vijiji
Mbalimbali na Kukagua Shughuli Mbalimbali za Vijana Kisha Kuwasili Mjini Njombe Majira ya Jioni Siku Hiyo.
Akiwa Mjini
Njombe Katibu Mkuu Kinana Atazindua Mradi wa Kitega Uchumi wa CCM na
Kufanya Mkutano wa Hadhara Katika Uwanja wa Roman Catholic Karibu na
Benki ya CRDB Hapo Disemba 7 Mwaka Huu.
Katika Kipindi Hiki Chama cha Mapinduzi CCM Taifa Kupitia Katibu Wake Mkuu Kimeendelea Kufanya Zaiara Katika Mikoa Mbalimbali Ambapo Hadi Sasa Msafara Huo Utawasili Mkoani Njombe Ukitokea Jijini Mbeya.
0 comments:
Post a Comment