Home » » MMOJA AFARIKI KWA SABABU YA UBOVU WA BARABARA MAKETE

MMOJA AFARIKI KWA SABABU YA UBOVU WA BARABARA MAKETE

Written By kitulofm on Tuesday, 31 December 2013 | Tuesday, December 31, 2013



Mtu mmoja aliyetambulika kwa jina la Modesta mkazi wa Ludewa amefariki dunia wakati akiwa njiani akikimbizwa katika hospitali ya Mission Ikonda kulingana na tatizo la barabara ya Makete-Njombe kuwa mbovu

Hata hivyo Mtu huyo aliyefariki dunia katika eneo kulingana na tatizo la ubovu wa barabara na gari kushindwa kupita kirahisi inasemekana kuwa hadi kufikia saa kumi na moja jioni kulikuwa na wagonjwa waliokuwa katika hali mbaya

Taarifa hizo zimetufikia mara baada ya barabara ya Makete Njombe eneo la Mang’oto kuanzia shule ya sekondari mang’oto hadi getini kutopitika hali inayopelekea wasafiri kushindwa kushindwa kufika kwa wakati katika eneo husika

Kwa taarifa za awali inaonyesha kuwa kuna wakandarasi wanakuja kufanya ukarabati ambapo nao wamekwama eneo hilo ikiwa tatizo kubwa ni kifusi kilichosambazwa katika eneo hilo ambapo hadi kufikia jioni ya leo gari zaidi ya 10 zilikuwa zimekwama katika eneo hilo


Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm