Home » » WATOTO WACHOMWA MIKONO NA BABA MZAZI

WATOTO WACHOMWA MIKONO NA BABA MZAZI

Written By kitulofm on Thursday, 5 December 2013 | Thursday, December 05, 2013

Watoto wawili wenye umri wa miaka tisa,wamechomwa moto viganja vyao vya mikono na baba zao katika wilaya ya Newala mkoani Mtwara.

Ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku kumi na sita za kupinga ukatili wa kijinsia hapa nchini, ITV kwa kushirikiana na chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA waliamua kufuatilia tukio la ukatili waliofanyiwa watoto hao kwa kuchomwa moto viganja vya mikono yao na baba zao walowazaa kwa kumtafuta kwanza afisa ustawi wa jamii wa wilaya ya Newala bwana George Martin Shinganya ili kueleza walichofanyiwa watoto hao katika vijiji tofauti vya wilaya hiyo.

ITV ililazimika kumtafuta mwalimu mkuu wa shule ya msingi Mwongozo katika kijiji cha Makonga kata ya Nambunga bwana Nurdin Machemba,na kueleza kuwa alishughulikia suala la mtoto huyo kama mwanafunzi wake na kisha kukabidhi uongozi wa serikali ya kijiji kuendelea nayo lakini mtuhumiwa amekimbilia nchi ya Msumbiji hivyo kuomba serikali kusaidia ili akamatwe.

chanzo:ITV
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm