Home » » JESHI LA POLISI WILAYANI MAKETE LIMESEMA MSIMU WA SIKUKUU HALI ILIKUWA SHWARI

JESHI LA POLISI WILAYANI MAKETE LIMESEMA MSIMU WA SIKUKUU HALI ILIKUWA SHWARI

Written By kitulofm on Saturday, 4 January 2014 | Saturday, January 04, 2014

Hali ya usalama katika wilaya ya Makete kwa msimu wa sikukuu za Krismas kwa mwaka 2013 na Mwaka mpya 2014 imeenda vizuri bila matatizo

Akitoa taarifa hiyo kwa wanahabari mapema hii leo ofisini kwake Mkuu wa polisi Wilaya ya Makete (OCD)Alfred Kasonde amesema kuwa msimu wa Krismas na mwaka mpya umeenda vizuri kwani hakuna tukio lolote la uvunjifu wa Amani lililoripotiwa katika kituo hicho

Hata hivyo katika mazungmzo hayo amesema kuwa wananchi na wakazi wa wilaya ya Makete wamesherehekea sikukuu hizo kwa amani,upendo na mshikamano kama ilivyotegemewa

Pia amesema kuwa Jeshi la polisi wilayani Makete lilijipanga vyema kuhakikisha amani inapatikana muda wote kwani Doria kutoka kwa jeshi hilo ilikuwa ikifanyika kwa msimu wote wa sikukuu hizo

Hivyo Kasonde amesemewashukuru wananchi kwa kusherehekea sikukuku hizo kwa kufuata taratibu na sheria bilashuruti kwani ni wajibu wa kila mmoja kulinda amani pamoja na kuwa na ushirikiano katika jamii inayotuzunguka

Hata ametoa wito kwa wananchi wilayani hapa kuendeleza amani,mshikamano pamoja na upendo na kuongeza kuwa Jeshi limejipanga  kuhakikisha kuwa amani inapatikana kwa wakati wote kuanzia mwaka 2014 na kuendelea

Na Furahisha Nundu

Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm