Home » » NMB MAKETE YATOA MSAADA KITUO CHA WATOTO YATIMA DENTAL

NMB MAKETE YATOA MSAADA KITUO CHA WATOTO YATIMA DENTAL

Written By kitulofm on Friday, 3 January 2014 | Friday, January 03, 2014



Kituo cha kulelea watoto yatima kilichopo chuo cha Dental ktk Tarafa ya Bulongwa tarehe mosi January 2014 kimepokea msaada wa vitu mbalimbali kutoka Benki ya NMB tawi la Makete wenye thamaani ya sh.laki 3

Akikabidhi msaada huo Meneja mahusiano kwa wateja wa Benki ya NMB-Makete Bw.Ally Sheyo amesema kama wafanyakazi wa benki hiyo wameamua kutoa msaada kwa watoto hao kwa sababu kituo hicho kinategemea misaada kutoka kwa wahisani

 
Mahitaji yaliyotolewa ni pamoja na mafuta ya kupikia,unga,sabuni na sukari ,Hata hivyo ametoa wito kwa taasisi binafsi na zile za serikali  kutembelea kituo hicho kwani kinakabiliwa na changamoto mbalimbali.


Kwa upande wake Mlezi wa watoto hao Bi.Sekela Nkyami ametoa shukrani kwa Benki hiyo  kwa moyo waliouonyesha na kuongeza kuwa anashukuru kwa msaada huo kwani kituo hicho kinaendeshwa kwa msaada wa Sister Anna ambaye anajitahidi kuomba misaada kwa wahisani na hakuna fungu lolote kutoka serikalini.

Pia ameongeza kuwa watu wa ustawi wa jamii wawe karibu na kituo hicho kwani ni wajibu wao kukitembelea kituo na kujitahidi kuomba misaada serikalini,kwa wahisani pamoja na kuwafikishia walengwa mara misaada hiyo ifikapo ili kuwasaidia watoto hao.

Na Fadhili Lunati
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm