Home » » MICHANGO YA WANANCHI ITASAIDIA KUJENGA MAABARA ZA SEKONDARI

MICHANGO YA WANANCHI ITASAIDIA KUJENGA MAABARA ZA SEKONDARI

Written By kitulofm on Saturday, 1 February 2014 | Saturday, February 01, 2014





Wito umetolewa kwa wananchi wa wilaya ya makete katika kuchangia ujenzi wa maabara katika  shule za sekondari zinazo wazunguka wananchi ili kuongeza kiwango cha elimu wilayani makete na Tanzania kwa ujumla.

Hayo yamesemwa na Afisa mtendaji wa kata ya mang’oto bw,Clemensi sanga,akiwa ofisini kwake huku akieleza kuwa
kwa mwaka 2014 kata hiyo imejipanga kuhakikisha kata hiyo inachangia loli 30 za mawe katika ujenzi wa maabara katika shule ya secondary Mang’oto lengo likiwa ni kuinua kiwango cha taaluma katika masomo ya sayansi,na kupata wataalamu wa sayansi wilayani hapa na nchini.

Bw,Sanga amesema kuwa sambamba na mipango hiyo shule hiyo inakabiliwa na changamoto mabalimbali ikiwemo nyumba za kuishi walimu,vyoo na bwalo kwa ajili ya kutumia wakati wa kula chakula.

Kwa upande wa wananchi wa kata ya mang’oto wame ishukuru halmashauri ya (w) ya makete kwa juhudi walizo fanya katika kuhakikisha  miundombinu ya shule hiyo pamoja na walimu wanapatikana tangu kuanzishwa kwa shule hiyo.


Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm