Home » » MZOZO KATI YA MTENDAJI WA KIJIJI NA WANANCHI MALEMBULI WILAYANI MAKETE UMEMALIZIKA NA MKURUGENZI WA WILAYA

MZOZO KATI YA MTENDAJI WA KIJIJI NA WANANCHI MALEMBULI WILAYANI MAKETE UMEMALIZIKA NA MKURUGENZI WA WILAYA

Written By kitulofm on Saturday, 1 February 2014 | Saturday, February 01, 2014

Mkurugenzi mtendaji wa harmashauri ya (w) yamakete bw,Iddy nganya ametoa rai kwa wannchi wa makete kuto jichukulia sheria mkononi pindi kunapokea sintofahamu juu ya uwajibikaji wa watendaji katika shughuri za kimaendeleo.

 Akizungumza na wananchi wa kijiji cha Malembuli  katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha malembuli kilichopo katika kata ya mang’oto katika kutafuta suluu ya mzozo ulio ibuka baina ya wananchi  na afisa mtendaji wa kijiji Bw, Nganya,amesema watendaji wote wanawajibu wa kusoma mapato na matumizi kwa wananchi ili kujua hali ya maendeleo katika eneo husika.

Sambamba na hatua hiyo Mkurugenzi wa Harmashauri ya (w) ameeleza umuhimu wa kusoma mapato na matumizi na kuwataka wananchi kutowafumbia macho viongozi wanao fanya kazi kwa uzembe kwa kuwa wao ndio wasimamizi wa shughuli za maendeleo

Katika mkutano  huo ulio udhuriwa na viongozi wa kijiji kata na wananchi kwa  ujumla ajenda ya mkutano huo ilikuwa ni kutafuta suluu ya mzozo ulio ibuka mwanzoni mwa mwezi wa kwanza mwaka huu ambapo wananchi wali taka kusomewa mapato na atumizi ya kijiji na trekta  kwa kipindi cha zaidi ya miezi 6 hawaku somewa mapato na matumizi.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji ambaye ndiye aliye tuhumiwa kutosoma mapato na matumizi amekiri kutokea kwa ucheleweshaji na kwamba sababu zilizopelekea kutosoma mapato na matumizi kwa kipindi hicho ni matatizo ya kifamailia ikiwemo misiba 3 iliyo mpata kwa  kipindi hicho.

Aidha watu sita wakiwemo vijana wameyakimbia makazi yao kwa kuhofia  kukamatwa na jeshi la polisi kwa tuuma za kuvuruga mkutano wa kijiji siku hiyo ya tukio. 



Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm