Home » » MACHAFUKO KIA WAMASAI WAGOMA KUHAMA KATIKA ENEO LA UWANJA WA NDEGE!

MACHAFUKO KIA WAMASAI WAGOMA KUHAMA KATIKA ENEO LA UWANJA WA NDEGE!

Written By kitulofm on Tuesday, 25 March 2014 | Tuesday, March 25, 2014

Jana majira ya sita mchana hadi saa kumi na moja jioni katika barabara iendayo uwanja wa ndege wa kimataifa KIA Kilimanjaro International Airport kumetokea machafuko pata shika vuta nikuvute shati kuchanika rubega kufumuka..!

Takribani kama masaa mawili usalama ulipotea baada ya Wamasai kudai kufukuzwa katika makazi yao wakiambiwa ni eneo la uwanja wandege.

Wamasai hao waliamua kuzuia magari yalioelekea Uwanjani hapo huku wakisema kuwa hata wamiliki wa uwanja huo nao wahame kwani waliwakuta awali wakiishi hapo.

 Polisi na magari ya PT walifika katika tukio hilo na kutaka kumaliza migogoro hiyo kisheria ila wamasai wamesema endapo muafaka utalenga kuwakandamiza hawako tayari kuhama.



CHANZO:EDDY BLOG Imeripotiwa na DJ TINDO WA UTS TAIFA KILIMANJARO
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm