Home » » MAGARI YENYE NAMBA BINAFSI YAZUIWA KUFANYA BIASHARA MJINI NJOMBE

MAGARI YENYE NAMBA BINAFSI YAZUIWA KUFANYA BIASHARA MJINI NJOMBE

Written By kitulofm on Friday, 21 March 2014 | Friday, March 21, 2014

Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Njombe RTO  James Kiteleki Akizungumza na Baadhi ya Viongozi wa Daladala na Taxi Mjini Njombe Ofisini Kwake.
Mwenyekiti wa Daladala Mkoa wa Njombe Bwana Seleman Mwenda Akitolea Ufafanuzi wa Kero Wanazo zipata Toka Kwa Madereva wa Taxi za Kusalaliza na Bajaji Mjini Njombe



Jeshi la  Polisi Mkoani Njombe Kupitia Kitengo cha Usalama Barabarani  Kwa Kushiririkiana   Mamlaka ya Udhibiti wa  Usafirishaji Wa nchi Kavu Na Majini  SUMATRA  Imepiga Marufuku  Utumiaji wa Namba Za Magari ya Binafsi Katika   Shughuli za Kibiashara na Kuwataka Kupeleka Orodha Ya Majina ya Madereva wa Taxi  "Wanaosalaliza" Ili Kuweza Kuwachukulia Hatua Madereva Hao.

Akiongea Kwenye Kikao na Wakuu wa  Vituo Vya Daladala, Bodaboda na Taxi  Kamanda wa Kitengo Cha Usalama  Barabarani RTO   James Kiteleki Amesema Kuwa  Kutokana na  Kufanyika kwa Vikao Vingi  Vyenye Kujadili  Suala Hilo Hivyo ni Muda Wa Kila Mtumiaji Wa Vyombo Vya Moto Kufuata Sheria.

Katika Hatua Nyingine  Afisa Mfawidhi wa Sumatra Mkoa Wa Njombe Bi Mary  Menard Amewataka Wale Ambao Hawajakidhi   Masharti  Ya Kuendesha Vyombo Vya Moto  Kupaki Vyombo Hivyo Ikiwemo  Kuwa na Namba ya Chombo Yenye Rangi ya Njano. 

Kwa Upande  Wao Baaadhi ya Viongozi wa Vituo vya Daladala na Taxi na Bodaboda   Licha ya Kuliomba Jeshi Hilo  Kusogeza Muda Mbele  Ili Kuwawezesha Wamiliki wa Vyombo Hivyo Kujipanga Lakini Baadhi Yao Akiwemo Kiongozi Wa Daladala  Wameonyesha Kulalamikia Madeleva Taxi Ambao Wamekuwa  Wakisalaliza  Wateja  na Kusababisha Abiria Kutokaa Kwenye Vituo  Maalumu vya Kupakia Abiria.

Kwa Upande Wake RTO Akilijibia Suala Hilo  Amewataka  Viongozi wa Vituo Vya Taxi  Kuwasilisha Majina ya Madeleva Wote Ambao Wamekuwa Wakivunja Utaratibu  Uliowekwa wa Kupaki katika Vituo Ili Kuweza Kuwashughulikia.

 Chanzo:Eddy blog
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm