Home » » MKUU WA SHULE YA SEKONDARI LUPALILO AKANUSHA TAARIFA ZA UPIGAJI PICHA ZA UTUPU KWA WANAFUNZI

MKUU WA SHULE YA SEKONDARI LUPALILO AKANUSHA TAARIFA ZA UPIGAJI PICHA ZA UTUPU KWA WANAFUNZI

Written By kitulofm on Monday, 3 March 2014 | Monday, March 03, 2014

Mkuu wa shule ya Sekondari Lupalilo Mwl.Liombo amekanusha Taarifa zilizozagaa kuhusiana na wanafunzi wa shule ya sekondari Lupalilo kupiga picha za utupu

Mkuu huyo amesema taarifa hizo si za kweli bali wanafunzi hao wamepiga picha ambazo haziendani na maadili ya shule za sekondari wilayani Makete na hapa nchini
Akizungumza na kitulo fm mapema hii leo katika kipindi cha Morning Power mara baada ya kupigiwa simu kutoa maelezo ya kina kuhusu taarifa zilizozagaa mitaani kuhusu wanafunzi wa shule ya Lupalilo iliyopo katika kata ya Tandala amesema kuwa taarifa hizo si sahii ukweli ni kwamba wamepiga picha ambazo ni tofauti na maadili mapoja na sheria za shule hiyo

Pia amesema kuwa hatua zilizochukuliwa dhidi yao ni pamoja na kuwaita wazazi wao na kufanya mkutano wa pamoja wazazi na watoto shule nzima kwani wanafunzi waliofanya kosa hilo ni wengi,baada ya hapo walipewa adhabu ya kuchapwa viboko na wazazi wao mbele ya wanafunzi wote wakiwepo wazazi na kupewa adhabu ya kukata kuni na kukwetua barabara mita kadhaa 

Na Furahisha Nundu


Share this article :

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

KITULO FM LOGO

KITULO FM LOGO
Tusikilize masaa 18 kwa siku kupitia masafa ya 97.0 FM ukiwa wilayani Makete mkoani Njombe na maeneo ya jirani

WASOMAJI WETU

KUMBUKUMBU YA HABARI ZETU

 

Copyright © 2013. KITULOFM BLOG - Haki zote zimehifadhiwa
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inawezeshwa na Kitulo Fm